SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jan 16, 2016

LEICESTER CITY YABANWA MBAVU NA ASTON VILLA

Leicester City imelazimishwa sare ya goli 1-1 ugenini dhidi ya Aston villa katika mchezo wa ligi kuu nchini England. Goli la Leicester City limefungwa na Okazaki katika dk ya 28 na goli la kusawazisha kwa upande wa Aston Villa limefungwa na Gestede dk ya 75. Kwa matokeo hayo  Leicester City inapanda kileleni mwa ligi hiyo kwa kufikisha point 44 nyuma ya Arsenal na Man City wenye point 43

AZAM YALAZIMISHWA SARE NA AFRICAN SPORTS

AZAM FC imelazimishwa sare ya
kufungana bao 1-1 na African Sports
ya Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu
ya Vodacom Tanzania Bara usiku huu
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi,
Dar es Salaam.
Sare hiyo inaiongezea Azam FC pointi
moja na kufikisha 36 baada ya mechi
14, ikiwazidi pointi tatu mabingwa
watetezi, Yanga SC walio katika
nafasi ya pili, ingawa wana mechi
moja mkononi.

Katika mchezo uliochezeshwa na refa
Jonesia Rukyaa wa Kagera
aliyesaidiwa na Ferdinand Chacha na
Julius Kasitu, hadi mapumziko Azam
FC walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Bao hilo lilifungwa na kiungo wa
zamani wa Yanga SC, Frank Raymond
Domayo dakika ya 28 kwa shuti la
umbali wa takriban mita 20, baada ya
kupokea pasi ya Nahodha John
Raphael Bocco.

Pamoja na kumaliza dakika 45 za
kwanza, wakiwa nyuma, lakini African
Sports walionyesha upinzani kwa
Azam FC na mara mbili walikaribia
kupata bao.

Kipindi cha pili, Sports iliyo chini ya
kocha wa zamani wa Simba SC,
Ramadhani Aluko iliongeza bidii na
kufanikiwa kusawazisha bao hilo
dakika ya 59 kupitia kwa Hamad
Mbumba aliyemalizia mpira wa
adhabu uliopigwa na Mwaita Gereza.
Baada ya bao hilo, timu hizo
ziliendelea kushambuliana kwa zamu
na kosakosa zilikuwa za pande zote
mbili.

Matokeo hayo yanaipunguza kasi
Azam FC katika mbio za ubingwa na
sasa, mabingwa watetezi, Yanga SC
wanaweza kurejea kileleni iwapo
watashinda dhidi ya Ndanda FC
kesho.
Kwa African Sports, sare hiyo ya
ugenini inakuwa ahueni katika
harakati zao za kujiepusha na balaa la
kushuka daraja.

Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi
Manula, Shomary Kapombe, Waziri
Salum/Farid Mussa dk62, Abdallah
Kheri, Serge Wawa, Erasto Nyoni,
Jean Baptiste Mugiraneza, Salum
Abubakar ‘Sure Boy’, John Bocco
‘Adebayor’, Frank Domayo/Mudathir
Yahya dk65 na Kipre Herman
Tchetche.

African Sports; Zakaria Mwaluko,
Mwaita Gereza, Khalifa tweve, Rahim
Juma, Juma Shemvuni, Ally
Ramadhani/James Mendi dk86,
Mussa Chambega, Pera Ramadhani,
Hamad Nathaniel, Hassan Materema/
Mohammed Mtindi dk47 na Rajab
Isihaka/Hussein Issa dk70.

MAN CITY YAUA CHELSEA HOII

Timu ya Manchester City imeibuka na ushindi wa goli 4-0 dhidi ya Crystal palace katika mchezo wa ligi kuu nchini England magoli ya City yamefungwa na Delph  dk 22 Aguero 41,68 Na goli LA mwisho lilifungwa Na David Silva dk 84
Matokeo mengine.
Chelsea imetoka sare ya goli 3-3 dhidi ya Everton magoli ya Chelsea yamefungwa Na Costa 64, Fabregas 66 Na Terry 90 Na magoli ya Everton yamefungwa Na Millarlas 55, More 90 Na goli LA kujifunga la Terry 50.

Bournemouth 3-0 Norwich

Southampton 3-0 West brom

Newcastle 2-1 West ham

TOTTENHAM YAITANDIKA SUNDERLAND BILA HURUMA

Kiungo wa Tottenham
Hotspur, Christian Eriksen akiteleza
chini Uwanja wa White Hart Lane
kushangilia baada ya kuifungia mabao
mawili timu yake katika ushindi wa
4-1 dhidi ya Sunderland leo. Mabao
mengine ya Spurs yamefungwa
na Mousa Dembele na Harry Kane
kwa penalti, wakati la Sunderland
limefungwa na Patrick van
Aanholt

MATOKEO YOTE YA LIGI KUU TANZANIA BARA LEO YAPO HAPA

Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara imeendelea hii Leo katika viwanja tofauti tofauti. Jijini Dar es salaam Simba imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Mtibwa sugar goli la timu ya Simba limefungwa na Hamisi kiiza mwanzoni mwa kipindi cha kwanza.
Matokeo mengine.
Coastal union 1-1 Maji Maji
Stand united 1-0 Kagera sugar
Jkt ruvu 1-5 Mgambo jkt
Mbeya city 1-0 Mwadui fc
Toto Africans 0-1 Prisons

KINACHOFANYA SAMATTA ACHELEWE KWENDA ULAYA NI HIKI HAPA

Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
RAIS wa klabu ya Nantes ya
Ufaransa, Waldemar Kita
amesikitishwa mno na kitendo cha
mshambuliaji wa kimataifa wa
Tanzania, Mbwan Ally Samatta
kukataa ofa ya kujiunga na klabu
yake, lakini hajakata tamaa kwa
sababu kijana huyo bado ni mali ya
TP Mazembe.
“Tungependa kumpata.
Inavyoonekana amesaini (KRC Genk).
Lakini ni mali ya klabu gani? Atakuwa
huru mwishoni mwa msimu? Mawakili
wangu wanalishughulikia hilo suala
kwa siku mbili, au tatu,”.
“Kama itakuwa poa, au hapana, vizuri,
mbaya sana, yote maisha,” amesema
katika safu ya Ocean Press.
Wakati huo huo, tovuti ya Gazeti la
Lequipe la Ufaransa limeandika,
Samatta mwenye umri wa miaka 24
sasa, amekwishasaini Mkataba wa
awali na KRC Genk ya Ubelgiji.
Na lakini akiwa na Mkataba na TP
Mazembe hadi Aprili 30, Mwanasoka
huyo Bora Anayecheza Afrika hawezi
kuruhusiwa kwa dau la chini ya Euro
Milioni 1.
Na wakati Samatta tayari amepatiwa
viza na Ubalozi wa Ubelgiji kwenda
kusaini klabu ya KRC Genk, Rais wa
Mazembe, Moise Katumbi amegoma
kusikikiliza kuhusu klabu hiyo ya Ligi
Kuu ya Ubelgiji.
Rais wa Nantes ya Ufaransa,
Waldemar Kita amesikitishwa na
Samatta kukataa ofa ya kujiunga na
klabu yake
BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE
inafahamu Katumbi anataka Samatta
aende Nantes FC ya Ligi Kuu ya
Ufaransa, ambayo amekwishafikia
makubaliano nayo.
Na wiki iliyopita Nantes FC ilituma
mwakilishi wake Dar es Salaam,
ambaye alifanya mazungumzo na
Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo
mbele ya Ofisa mmoja wa Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF).
Katika mazungumzo, Kisongo alifikia
makubaliano ya maslahi binafsi na
Samatta ikiwemo dau la kusaini,
mshahara, masharti na marupurupu
mengine.
Kisongo alitaka kiwepo kipengele cha
mchezaji kutorejeshwa Afrika iwapo
hatapata nafasi ya kucheza Nantes,
bali auzwe klabu nyingine ya Ulaya na
ikakubaliwa.
Nantes ilionyesha nia ya dhati kabisa
ya kumchukua Samatta na Kisongo
aliinuka kwenye meza ya
mazungumzo akiwa amekubali na
kusema anakwenda kuzungumza na
mchezaji.
Hata hivyo, inaonekana Samatta
mwenyewe ndiye anayetaka kwenda
Ubelgiji na si Ufaransa, kwani kitendo
cha Kisongo kutorejesha majibu kwa
Nantes kinaashiria ameshindwa
kumshawishi mchezaji wake akubali
ofa hiyo.
Wakati huo huo, Rais wa Mazembe
hayuko tayari kumuuza Samatta
Ubelgiji na yuko tayari kuona Samatta
anabaki Mazembe kumalizia Mkataba
wake ili aondoke kama mchezaji huru
Aprili, hali ambayo itamlazimu kusubiri
hadi Agosti kusaini Genk.
Kwa sasa, kambi ya Samatta inajaribu
kuomba msaada kwa viongozi wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, wakazungumze na Katumbi
ili akubali kumuacha mchezaji aende
klabu aliyochagua.
Rais Mstaafu, Dk Jakaya Mrisho
Kikwete ambaye kwa sasa ni
Mwenyekiti wa chama tawala, CCM,
Waziri wa Michezo, Nape Nnauye kwa
pamoja wameahidi kumsaidia Samatta
katika suala la kumlainisha Katumbi
akubali kupokea ofa ya Genk.
Wakati huo huo, Nantes wamekuwa
wakimpigia simu Kisongo wakisema
wanamsubiri mchezaji aende kusaini,
lakini Meneja huyo anakosa majibu ya
uhakika.
Inaonekana tayari Katumbi anaujua
mchezo wote unaoendelea naye
ameamua kukaa kimya akiamini
Samatta hawezi kufanya chochote
kwa sasa bila baraka zake.
Na wazo la kusema Samatta asubuhi
hadi Aprili atakapomaliza Mkataba
wake ili asaini kama mchezaji huru
Agosti halifurahiwi hata na Kisongo
mwenyewe.
Samatta aliyejiunga na TPM mwaka
2011 akitokea Simba SC aliyoichezea
kwa nusu msimu, akitokea African
Lyon, hadi sasa ameichezea klabu
hiyo mechi 103 na kuifungia mabao
60.
Ndani ya mechi hizo, kijana huyo wa
umri wa miaka 24, ameshinda taji la
Ligi ya Mabingwa Afrika na Mazembe,
huku naye akiibuka mfungaji bora wa
michuano hiyo na kutwaa tuzo ya
Mchezaji Bora Anayecheza Afrika.

ALI KIBA: SIO KWELI KUWA DIAMOND PLATNUMZ NDIE ANAEPITISHA VIDEO ZA BONGO KWENYE KITUO CHA MTV

Siku kama mbili zilizopita kulikuwa na habari
iliyokuwakuwa maarufu sana, ni kuhusu kauli ya
Diamond Platnumz akisema kuwa video yoyote
ya Bongo haipigwi katika Kituo cha MTV bila
yeye kushirikishwa, leo Ali Kiba kaamua kumjibu
kwa kusema kuwa hana uhakika na kauli hiyo
ya Diamond Platnumz.
Katika kipindi cha XXL katika kipengele cha 255
Ali kiba amesema “ Nitawaambia ukweli ambao
unawahusu, kama ni kweli watakuwa wanakosea
(MTV), haikai sawa na sidhani kama ni
kweli….Yaani haikai sawa na sidhani kama ni
kweli, kwasababu watakuwa hawako fair, ndio
hivyo hawako fair, hajabeba talent ya kila mtu
(Diamond), kila mtu ana kipaji chake na kila mtu
ana haki ya kuonesha kipaji chake kazi yake.
Unajua kila mtu anafanya biashara ya muziki
saizi, sio mtu anafanya masihara unapoona mtu
anafanya video yake anagharamikia unajua
haipendezi, kwahiyo sidhani kama ni kweli……. “.

ALICHOSEMA KOCHA MATOLA BAADA YA SIMBA KUMFUKUZA KOCHA

Matola, amesema Simba imechelewa
kumtimua Kocha Dylan Kerr kwani alianza
muda mrefu kutibua mambo.
Hivi karibuni Matola aliamua kuondoka
mwenyewe Simba na kujiunga na Geita
Gold Sports ya Ligi Daraja la Kwanza kwa
kile kilichoelezwa kuwa ni kutoelewana
kwake na Kerr ambaye ni raia wa
Uingereza.
Simba mapema wiki hii ilitangaza rasmi
kuvunja mkataba na Kerr kwa
kilichoelezwa kutoridhishwa na mwenendo
wa kikosi hicho katika mechi zake za
michuano mbalimbali.
Matola alisema: “Kerr ni kocha mzuri ila
nilishawaambia viongozi mapema kuwa
hafai ndani ya timu kutokana na yeye
kutaka kufuata kile anachokiamini bila ya
kushirikiana na wenzake hata kama
anakosea.
“Simba imechelewa kumtimua kwani
ameiweka timu mahali pabaya na kama
angeondoka mapema usikute klabu
ingekuwa pazuri sasa,” alisema Matola.

AZAM FC NA AFRICAN SPORTS NI USIKU LEO CHAMAZI

MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara kati ya vinara, Azam
FC na African Sports ya Tanga
itachezwa kuanzia Saa 1:00 usiku
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi,
Dar es Salaam.
Leo kutakuwa na jumla ya mechi tatu
za Ligi Kuu, Dar es Salaam, moja
Uwanja wa Karume kati ya JKT Ruvu
na JKT Mgambo na nyingine Uwanja
wa Taifa, kati ya Simba SC na Mtibwa
Sugar.
Na ili kuwapa fursa watu kuona mechi
zote mbili kubwa za leo kupitia Azam
TV, ndiyo maana mchezo mmoja wa
Dar es Salaam umepelekwa usiku.
Ikumbukwe Azam FC iliyo kileleni
mwa Ligi Kuu kwa pointi zake 35
baada ya kucheza mechi 13,
ikifuatiwa na mabingwa watetezi,
Yanga SC wenye pointi 33 za mechi
13 pia, imepania kushinda mechi hiyo
ili kuzidi kupiga kasi katika mbio za
ubingwa.
Baada tu ya kutolewa katika Kombe
la Mapinduzi visiwani Zanzibar wiki
iliyopita, Azam FC ilirejea Dar es
Salaam mapema kuanza maandalizi
ya mechi dhidi ya Sports.
Na katika kipindi hiki kifupi
wamefanya hadi mazoezi ya ufukweni
kuhakikisha wachezaji wake
wanakuwa fiti kikamilifu.
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo ni
baina ya mabingwa wa zamani wa ligi
hiyo, Simba SC na Mtibwa Sugar
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
kuanzia Saa 10:00 jioni.
Mabingwa hao wa zamani wa Ligi
Kuu, wanakutana Jumamosi ya leo
ikiwa ni wiki moja tangu wakutane
katika Nusu Fainali ya Kombe la
Mapinduzi visiwani Zanzibar, Mtibwa
Sugar ikiilaza Simba SC 1-0, bao
pekee la Ibrahim Rajab ‘Jeba’.
Na baada ya kipigo hicho, Simba SC
iliwafukuza makocha wake,
Muingereza, Dylan Kerr na Mkenya
Iddi Salim na sasa Mganda, Jackson
Mayanja ndiye yupo na timu.
Mtibwa Sugar nao wataingia katika
mchezo wa kesho wakiwa na
kumbukumbu ya kufungwa mabao 3-1
na URA ya Uganda katika fainali ya
Kombe la Mapinduzi Jumatano.
Mechi nyingine za ligi hiyo leo ni kati
ya JKT Ruvu na Mgambo JKT Uwanja
wa Karume, Dar es Salaam, Toto
Africans na Prisons Uwanja wa CCM
Kirumba, Mwanza, Stand United na
Kagera Sugar Uwanja wa Kambarage,
Shinyanga, Mbeya City na Mwadui FC
Uwanja wa Sokoine, Mbeya na
Coastal Union na Majimaji wa Uwanja
wa Majimaji, Songea.
Ligi Kuu itaendelea kesho kwa mechi
moja tu, mabingwa watetezi, Yanga
SCwakiikaribisha Ndanda FC Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga SC nayo inarejea kwenye Ligi
Kuu baada ya kutolewa katika Nusu
Fainali ya Kombe la Mapinduzi,
wakifungwa kwa penalti 4-3 na URA
kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika
90.